vodacom.co,tz

vodacom.co,tz

Alhamisi, 18 Desemba 2014

Johari: Kizazi Changu Kinafanya Kazi Namsubiri Mwanaume wa Kunifungua tu Akishanioa

Johari: Kizazi Changu Kinafanya Kazi Namsubiri Mwanaume wa Kunifungua tu Akishanioa

Na Laurent Samatta
PAMOJA na tetesi kuwa nguli wa filamu za Kibongo Blandina Chagula ‘Johari’, ameshindwa kushika mimba, mwenyewe ameamua kufunguka na kudai kuwa kizazi chake kinafanya kazi na anachosubiri ni kumpata mwanaume ambaye atakuwa tayari kumuoa ndipo atakaporuhusu kuzalishwa.

Akizungumza na Amani, Johari alisema kuwa endapo akitokea tayari yupo ndani ya ndoa anaweza kufanya hivyo lakini kwa maneno ya watu kamwe watasubiri kwani anaamini kizazi chake kipo imara na wakati wowote akiamua kushika mimba kitafanya kazi.

“Kizazi changu kinafanya kazi na mipango hiyo ya kushika mimba mimi siwezi kukubali nipate mtoto kabla ya kuolewa, suala la kufanya jambo kwa lengo la kuwafurahisha watu mimi siwezi kufanya hivyo,” alisema Johari.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni