vodacom.co,tz

vodacom.co,tz

Jumanne, 1 Novemba 2016

Unamshauri Nini Diamond Katika Ngoma yake na Rich Mavoko Inayokuja?


Aisee kwanza huyu jamaa anastahili Hongera nyingi sana, Huyu ni identity ya taifa kwa sasa within and outside of Africa.

Huyu jamaa pia ana busara na moyo wa kiume sio wa kulialia, juzi alipokosa award ktk MTV awards aliwapa moyo wasanii wenzake wa kitanzania katika ujumbe aliouandika instagram kutokata tamaa kwani watazichukua tu.

Ingawa atakuwa busy sana mpaka mwakani ila Salam amesema kuwa Diamond bado anatoa nafasi kwa watanzania kumshauri afanye nini ili kuboresha mara dufu nyimbo zake hususan videos.

Katika kundi la Wasafi Classic Baby (WCB), Diamond Platnumz ameishaimba na

Harmonize wimbo wa BADO

Rayvanny wimbo wa SALOME

wimbo utakaofuata ataimba na Rich Mavoko (pacha wake kisauti)

Unamshauri nini SIMBA?

Mimi namshauri kwanza katika video yake asimtumie Mwanamke wa kizungu as his Video Queen.

Kuna mabinti wa kiafrika hasa wa kitanzania wazuri sana tu na inapendeza akiwatumia hao na sio wazungu.

Toa ushauri wako wa kuboresha kazi ya Platnumz.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni