vodacom.co,tz

vodacom.co,tz

Jumanne, 11 Aprili 2017

Kuhusiana na Tetesi Kuwa Amelipwa Dola 5000 Ili Kusema Tofauti na Ukweli..Roma Kafunguka Haya Huku Akilia..!!!

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Roma Mkatoliki amezungumza kwa hisia juu ya wasanii wenzake na watu wengine ambao wanahusisha kutekwa kwao na mchezo wa kiini macho.
“Watu wanasema tunatumika kisiasa tunataka kuichafua Serikali, wapo wanaosema tunatafuta kiki na kuna wengine wamekwenda mbali zaidi na kudai tumelipwa Dola 5,000 ili tutengeneze habari hii.
“Tunaumizwa sana na kauli hizo, nguvu za watu walizotumia kupaza sauti zao halafu watu wanasema tunacheza mchezo, hatuwezi kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya fedha sisi ni watu wa kawaida sana familia zetu ni masikini, lakini hatuwezi kukubali kuumizwa hivi kwa ajili ya fedha.”
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe amesema anataka kupata majibu ya tukio la utekaji wa Roma Mkatoliki kabla ya kuwasilisha bajeti yake bungeni.
“Mimi nitakuwa kwa wapelelezi, nataka kujua suala hili nipate majibu kabla sijawasilisha bajeti yangu bungeni ili bajeti yangu ipite bila makelele mengi,” amesema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni