Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Roma Mkatoliki amezungumza kwa hisia 
juu ya wasanii wenzake na watu wengine ambao wanahusisha kutekwa kwao na
 mchezo wa kiini macho.
“Watu wanasema tunatumika kisiasa tunataka kuichafua Serikali, wapo 
wanaosema tunatafuta kiki na kuna wengine wamekwenda mbali zaidi na 
kudai tumelipwa Dola 5,000 ili tutengeneze habari hii.
“Tunaumizwa sana na kauli hizo, nguvu za watu walizotumia kupaza sauti 
zao halafu watu wanasema tunacheza mchezo, hatuwezi kuhatarisha maisha 
yetu kwa sababu ya fedha sisi ni watu wa kawaida sana familia zetu ni 
masikini, lakini hatuwezi kukubali kuumizwa hivi kwa ajili ya fedha.”
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe 
amesema anataka kupata majibu ya tukio la utekaji wa Roma Mkatoliki 
kabla ya kuwasilisha bajeti yake bungeni.
“Mimi nitakuwa kwa wapelelezi, nataka kujua suala hili nipate majibu 
kabla sijawasilisha bajeti yangu bungeni ili bajeti yangu ipite bila 
makelele mengi,” amesema.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni