vodacom.co,tz

vodacom.co,tz

Jumatatu, 10 Aprili 2017

Zitto: Nimetonywa Kuna Mpango wa Watu Saba Kutekwa Wakiwamo Mimi na Mawaziri Watatu...!!!!



Kama muelewavyo story za kuteka na kutaka kutekwa zimepamba moto na kila mtu hasa wabunge wanasema wanataka kutekwa.
janakwenye kipindi cha DW alitafutwa mbunge Zitto kuzungumzia hili swala kwanza aliulizwa kama ana taarifa ya bashe kusema kuna wabunge 11 wanatafutwa kutekwa akasema hana taarifa kamili na ni vigumu yeye kulielezea na alisema kuwa yeye binafsi alitonywa kuwa kuna watu saba nje ya bunge, wabunge na mawaziri watatu wanapangwa kutekwa....
Lakini Zitto aliulizwa una uhakika gani na vyanzo vyako kama havikudanganyi? alisema yeye ametonywa na ana haki ya kuchukua tahadhari.. hata hivyo aliulizwa mbona taarifa zake na mbunge wa Nzega zinakindhana mwenzie anasema watu 11 na yeye anasema watu 7 wakiwemo mawaziri? Zitto alijibu kwa kusema yeye hajui vyanzo vya bashe vilivyo mpa taarifa ila yeye ana vyanzo vyake hivyo siwezi jua vyanzo vya Mh Bashe.
Pia Mh Zitto aliulizwa kama anamjua muhusika wa utekaji huu akasema angekuwa anamjua asingelipiga kelele na wala isingekuwa mjadala tena...
Pia Mh Zitto alisema kuwa yeye kesho atawasilisha hoja bungeni kutaka waunde kamati maalum ya kuchunguza matukio hayo ya utekaji na lazima watu wawajibike
Source: DW(6:00-6:30 PM)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni