"Jamani Pombe sio chai" - LULU asisitiza, adai anaiogopa zaidi ya ukoma.
MSANII wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’
amesema kuwa sasa hivi anaiogopa na kuiheshimu sana pombe akiamini
kwamba ndiyo chanzo cha maisha kuharibika.
Kwa mujibu wa tovuti ya GPL hivi , Lulu alisema tangu ametoka
gerezani ameamua kujiweka pembeni na kilevi hicho na kwamba bora aitwe
mshamba.
“Kiukweli nikiiona pombe kuna wakati naipa shikamoo kwani ndiyo
kichocheo cha kila baya hapa duniani, watakaoniona mshamba kwa
kubadilika kwangu wanione hivyohivyo,” alisema Lulu.
Msanii huyo kipindi cha nyumba alikuwa hakamatiki kwa kilevi na
kuna wakati aliwahi kuzimika alipofakamia pombe za ofa alipokuwa ndani
ya Ukumbi wa Maisha Club, jijini Dar.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni