BREAKING NEWS: JUMBA LA BIG BROTHER LATEKETEA KWA MOTO..SHOW YASOGEZWA MBELE!
Moto mkubwa umeikumba M-Net’s Big Brother Africa Hotshots house katika Studio ya Sasani na kusababishwa kusitishwa uzinduzi wa msimu
wa 9 wa Big Bother ambao ulibidi uanze tarehe 7 September siku ya
Jumapili. Hakuna mtu aliyepata madhara japokua chanzo cha moto huo bado
hakijajulikana na uchunguzi unaendelea.
Kwa sasa kampuni ya Endemol inayotengeneza kipindi hiki inatafuta jumba jingine ambalo watakaa housemates wa msimu mpya japokua wanasema linawaingizia gharama kubwa kimiundombinu na kufunga mitambo ya Camera.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni