Kaka wa Roma Mkatoliki, msanii wa muziki wa kizazi kipya aliyetekwa
akiwa na wenzake na kurejeshwa juzi, amesema watekaji waliwafunga
vitambaa vyeusi usoni, lakini hadi sasa hawawajui wahusika na
waliwarejesha na kuwaacha Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam.
Pia, kaka huyo, Omari Musa amesema Roma, ambaye alipata umaarufu kwa
nyimbo zake za kukosoa ukandamizaji wa vyama vya upinzani hasa katika
wimbo wa “Viva Roma”, hakuwa anarekodi wimbo mpya kama inavyodhaniwa.
Licha ya polisi kukana kuwa watu hao hawakuwa wanashikiliwa katika kituo
chochote cha polisi, Roma na wenzake walionekana Kituo cha Polisi
Oyesterbay, Kinondoni ambako walihojiwa kwa zaidi ya saa sita baadaye
kupelekwa Hospitali ya Mwananyamala.
Baada ya kutoka, Roma alizungumza kwa kifupi akiwashukuru Watanzania na
kusema atazungumza na wanahabari leo. Lakini, Musa alisema Roma hayupo
tayari kuzungumza mambo mengi yaliyompata au alichofanyiwa na watekaji
hao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni