UNAFIKI TUPA KULE...HUU NDIO UKWELI KUHUSU DIAMOND PLATINUMZ...!WASANII MNAJIFUNZA NINI TOKA KWAKE?! UNAFIKI TUPA KULE...HUU NDIO UKWELI KUHUSU DIAMOND PLATINUMZ...!WASANII MNAJIFUNZA NINI TOKA KWAKE?!
KWENU,
Wasanii wote wa Tanzania. Hongereni kwa kazi na namna mnavyojituma kupitia sanaa zenu. Ni jambo zuri tena la kujivunia maana mmetambua vipaji vilivyo ndani yenu na kuvitumia kujipatia riziki. Kwa upande wangu, naendelea vizuri. Nawatakia heri wasanii wote Waislam walio kwenye funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhan. Ni mwezi ambao kwa hakika, tunahitaji kuwa na subira na utulivu wa hali ya juu. Nimeona ni vyema leo nizungumze na wasanii wote kwa pamoja. Ndugu zangu, katika kila kinachofanywa na binadamu, kama akitaka kiwe na mafanikio ni lazima kuwe na juhudi, ubunifu, nia na malengo. Unaweza kuwa na vyote au kimojawapo ambacho kwa hakika kitakusaidia kupata vingine kisha kupaa kwenye kilele cha mafanikio. Hapa nitoe mfano mmoja mzuri sana kwa Diamond. Huyu bwana mdogo hana muda mrefu sana kwenye game.
Wasanii wote wa Tanzania. Hongereni kwa kazi na namna mnavyojituma kupitia sanaa zenu. Ni jambo zuri tena la kujivunia maana mmetambua vipaji vilivyo ndani yenu na kuvitumia kujipatia riziki. Kwa upande wangu, naendelea vizuri. Nawatakia heri wasanii wote Waislam walio kwenye funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhan. Ni mwezi ambao kwa hakika, tunahitaji kuwa na subira na utulivu wa hali ya juu. Nimeona ni vyema leo nizungumze na wasanii wote kwa pamoja. Ndugu zangu, katika kila kinachofanywa na binadamu, kama akitaka kiwe na mafanikio ni lazima kuwe na juhudi, ubunifu, nia na malengo. Unaweza kuwa na vyote au kimojawapo ambacho kwa hakika kitakusaidia kupata vingine kisha kupaa kwenye kilele cha mafanikio. Hapa nitoe mfano mmoja mzuri sana kwa Diamond. Huyu bwana mdogo hana muda mrefu sana kwenye game.
Ameibuka juzijuzi tu, lakini kutokana na juhudi, ubunifu, nia na malengo amefanikiwa na anazidi kupaa kimafanikio. Diamond tangu ameanza na kibao chake cha kwanza kabisa alijitahidi kuendelea kuongezeka na siyo kupungua. Hiyo ndiyo sababu kubwa iliyomfanya mpaka sasa anafanya vizuri kimataifa. Kwa bahati mbaya sasa, wapo baadhi ya wasanii (hasa wa muziki wa Bongo Fleva) wanamuonea kijicho! Nasisitiza baadhi.
Hawafurahishwi na mafanikio yake. Mbaya zaidi, sumu imesambaa sasa mpaka kwa baadhi ya mashabiki. Chuki tu! Kwa nini yeye? Kwa nini afanikiwe kimuziki? Kwa nini aorodheshwe kwenye kugombea tuzo? Kwa nini? Kwa nini?!
Diamond aliposhindwa kutwaa Tuzo za MAMA zilizofanyika hivi karibuni nchini Afrika Kusini, baadhi ya watu waliandika mambo ya ajabu sana kwenye mitandao ya kijamii.
Wengine walifikia hatua ya kusema kuwa, eti kama Diamond angeshinda watu wasingekunywa maji! Huo ulimbukeni tunaupata wapi ndugu zangu? Diamond ni nani? Jibu ni rahisi tu. Ni Mtanzania.
Anapokwenda
kushiriki tuzo za kimataifa anasimama kama Mtanzania. Hiyo ndiyo sababu
hata rais wetu, Dk. Jakaya Kikwete aliona umuhimu na akampongeza maana
aliwakilisha taifa. Kuwa
kwenye kinyang’anyiro pekee ni ushindi tosha. Kuna wasanii wangapi
Afrika? Kwa nini amechaguliwa yeye? Kwa nini si wengine? Kwa nini
hukuchaguliwa wewe? Kama
una roho hiyo ya korosho, achana nayo. Ni ushamba. Piga kazi
utafanikiwa. Kwanza Mungu hawezi kumsaidia mtu ambaye ana roho mbaya,
asiyependa mafanikio ya mwenzake. Safisha
moyo wako, fanya kazi kwa bidii, ongeza ubunifu, angalia soko
linahitaji nini, kisha achia kitu hewani – utavuma! Bila shaka ndivyo
anavyofanya Diamond.
Juzi
tu ametoka Marekani alipokuwa akishiriki kwenye Tuzo za BET. ni
mafanikio hayo. Lakini kwa sababu ni tuzo za kimataifa, hatuwezi kusema
ni mafanikio yake peke yake. Ni mafanikio ya wasanii wote wa Tanzania. Mafanikio
ya Watanzania wote. Ni mafanikio yetu. Kwa nini asipongezwe? Kwa nini
tusijipongeze? Kwa nini tusijifunze kupitia kwake? Chondechonde wenye
roho za kwa nini, hazina maana, pambaneni. Ukiona
rafiki yako amenunua gari zuri, usiumie – iwe changamoto kwako na ikupe
hasira ya kusaka mafanikio. Hata ukichukia, hakuna kitakachobadilika,
sanasana utakonda bure!
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni